Wednesday, October 10, 2012

Waziri Mkuu, Mkuu Mizengo Pinda Alipokutana na wajumbe wa Kituo cha

Waziri Mkuu, Mkuu Mizengo Pinda akiwa na wajumbe wa Kituo cha Demokrasia (TCD) baada ya kuzungumza nao Ofisini kwake jijini Dar es salaam Oktoba 8, 2012. Wejumbe hao ni viongoazi wa vyama mbali mbali vya siasa nchini.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
 Mwenyekiti wa Tume Ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora Jaji Kiongozi (Mstaafu) Amiri Ramadhan Manento (katikati) akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani jijini Dar es Salaam leo wakati akitoa muhtasari wa taarifa ya Uchunguzi wa Tume yake kuhusu tukio lililopelekea kifo cha Daudi Mwangosi kilichokea Septemba 2, 2012 kijijini Nyololo. Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa. (Kushoto) ni Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mahfoudha.A. Hamid na (kulia) ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kutoka Tume hiyo Florida Kazora.
 Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mahfoudha.A. Hamid  akizungumza wakati tume hiyo ilipokutana na waandishi wa habari leo
Baadhi ya waandishi wa habari walioshiriki kwenye mkutano huo.Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO

Monday, October 8, 2012

Ripoti Za Kifo Cha Mwangosi Kuwekwa Hadharani Leo



Na: Elizabeth Edward, Mwananchi.

 SERIKALI leo inatoa hadharani ripoti ya Kamati iliyoundwa kupata taarifa kuhusu vurugu zilizotokea mkoani Iringa na kusababisha kifo cha aliyekuwa mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Daudi Mwangosi. Wakati ripoti hiyo ikitarajiwa kutolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, Kamati nyingine iliyoundwa na Baraza la Habari (MCT) na Jukwaa la Wahariri Tanzania (Tef), nayo leo inatarajiwa kuweka hadharani ripoti yake.

 Kamati hizo ziliundwa kwa nyakati tofauti baada ya vurugu zilizotokea Septemba 2, mwaka huu katika Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi wakati polisi walipowatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakifungua tawi la chama hicho katika kijiji hicho. 

 Juzi, Makamu Mwenyekiti wa Kamati iliyoundwa na Dk Nchimbi, Theophil Makunga alimkabidhi waziri huyo na kusema Kamati yake ilifanya ziara Iringa na pia mahojiano na wadau mbalimbali Dar es Salaam.Kamati ya Nchimbi ilikuwa ikiongozwa na Mwenyekiti Jaji Steven Ihema, Makunga na Ofisa wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Pili Mtambalike, Kanali Wema Wapo wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) pamoja na Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi, Isaya Mngullu.

Tofauti na taarifa nyingine, ripoti ya mauaji ya Mwangosi inatarajiwa kutolewa hadharani ili umma uweze kuisoma, kuichambua na kutoa maoni kuhusu hatua za kuchukua ili matukio ya aina hiyo yasitokee tena. Ripoti ya MCT Katibu Mkuu wa Tef, Neville Meena alisema timu ya uchunguzi imeshamaliza kazi yake na leo itatoa rasmi ripoti kuhusiana na mazingira ya kifo cha Mwangosi.

Kamati hiyo iliundwa na watu watatu, John Mirenyi kutoka MCT, Hawra Shamte kutoka Tef na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Saimon Berege. “Sisi tukiwa wanahabari tuliunda Kamati yetu ili ifanye uchunguzi kuhusiana na mauaji ya mwanahabari mwenzetu, baada ya kukamilisha uchunguzi huo, sasa tupo tayari kuiwasilisha ripoti yetu hadharani,” alisema Meena. 

Chanzo:  http://www.mwananchi.co.tz

Mtumishi Wa Papa Ahukumiwa Kifungo ha miezi 18 jela





Mtumishi wa zamani wa Papa Benedict amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja na nusu kwa kuiba nyaraka za siri kutoka fleti ya Papa. 

Paolo Gabrieli na Papa Benedict Katika kujitetea mbele ya mahakama ya Vatikani, Paolo Gabriele alisema alifichua nyaraka hizo za siri kwa mwandishi wa habari kwa sababu akitaka kuonesha kile alichosema ni rushwa ovu ilioko katikati ya Kanisa la Katoliki. Msemaji wa Vatikani, Federico Lombardi, alieleza kuwa inavoelekea Papa atamsamehe mtumishi wake.

Uzinduzi Kampeni Za Udiwani CHADEMA Arusha


 Mgombea wa CHADEMA
Nassari akihutubia

Maelfu ya wananchi.jana jioni

Ajali Yaua watu Wawili Papohapo


Dereva wa Bodaboda na abiria wake, ambao hawakuweza kufahamika majina yao kwa haraka, wakiwa wamelazwa pembeni mwa barabara ya Bagamoyo eneo la Makongo, baada ya kugongwa na gari aina ya Starlet yenye namba za usajiri T 838 BKB, wakati wakiwa katika Pikipiki yao yenye namba za usajiri T 491 BFY, na kufariki dunia papo hapo. Ajali hiyo ilitokea jana asubuhi, Pichani ni raia akijaribu kutambua mwili wa marehemu katika ajali hiyo.

Sunday, October 7, 2012

Kardinali Rugambwa azikwa mara ya pili Bukoba

Anaonekana Baba Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini mara tu baada ya kukagua gari litakalo tumika kubebe mwili wa marehemu Kardinali Rugambwa
 Muonekano wa ndani ya Gari.
Muonekano wa gari litakalo ubeba mwili wa Marehemu Kardinali Rugambwa likiwa tayari limepambwa Maua.
 Mtangazaji wa kipindi cha dini, TBC katika kuwajibika
 Mzee Dioniz Malinzi akiteta jambo na Askofu Kilaini.
 Kila baada ya muda ndivyo wanavyozidi kuwasili Viongozi mbalimbali wa dini .
 Kikundi cha Ngoma kutoka nchini Burundi kikiendelea  na mashamsham  katika mahadhimisho haya.
 Shamrashamra za hapa na pale zikiendelea.
 Wadau na waumini wakikiristo wakifurahia burudani ya ngoma kutoka Nchini Burundi.

kuelekea ndani ya kanisa kuu.

 Mwili ukiingizwa ndani ya kanisa kuu katoliki Jimbo la Bukoba

 Heshima ya mwisho katika katika ktabaruku mwili wa Kardinali.
 Hapa nashindwa nielezeje ingawa naamini ni mwanzo wa ukurasa mwingine  katika kuendeleza  historia ya Marehemu Kardinal Rugambwa.


Monekano wa kaburi jipya ndani ya kanisa kuu, na pembeni yake zipo kaburi nyingine tatu.

 MISA IMEONGOZWA NA ASKOFU MKUU JIMBO LA MWANZA YDATHADEI RUAICH NA KUSAIDIWA NA NESTORIUS TIMANYWA.


Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda mara tu baada ya kuwasili mjini bukoba
 Watu na matukio,hapa waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari wakiwajibika
 Watu walioandaliwa maalum wakiwa wamebeba jeneza lililo na masalia ya Kardinali Laurean Rugambwa yatari kuingizwa katika Kanisa Kuu la Jimbo la Bukoba, la Bikira Maria wa Huruma kwa maziko.




Jeneza hilo lilokuwa na masalia likiwa limebebwa juu.

Na Theonestina Juma, Bukoba
MAELFU ya waumini wa Kanisa Katoliki kutoka ndani na nje ya nchi wamejitokeza kushiriki maziko rasmi ya masalia ya Kardinali wa Kwanza Mwafrika,Laurean Rugambwa yaliofanyika jana mjini Bukoba.
Misa ya kuombea masalia ya Kardinali huyo yalioongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza,Mhashamu Jude Thadeus Ruwa'ichi, katika Parokia ya Kashozi alikokuwa amezikwa kwa muda kutokana na Kanisa kuu la Bukoba la Bikira Maria wa Huruma aliloanza kujenga mwenyewe akiwa hai na kutaka azikwe lilikuwa likifanyiwa ukarabati mkubwa uliochukua takribani miaka 10.
Katika misa hiyo ilioendeshwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza, Mhashamu Jude Thadeus Ruwa’ichi yamehudhuriwa na maaskofu zaidi ya 30 kutoka katika majimbo mbali mbali hapa nchini pamoja na miamia ya mapadri pamoja na watawa
Katika parokia ya Kashozi kutokana na uwingi wa watu waliojitokeza kushiriki katika misa ya ililazimika geti la kuingilia kanisani kufungwa kwa muda kwa kuhofia kungeweza kutokea watu kukanyagana, ambapo geti hilo lilifunguliwa wakati wa kukominika.
"Naomba geti la lango kuu lililokuwa limefungwa lifunguliwe kwani kwa sasa ni wakati wa kukomunika"alisikika Padri mmoja akitoa maelekezo.Akihubiri katika misa hiyo ya kuhamisha masalia ya Kardinali Rugambwa,Mhashamu Ruwa'ichi alisema kila Askofu wa jimbo wa Kanisa hilo wanayo haki ya kuchagua azikwe wapi.
Alisema hata Kardinali Rugambwa angependekeza azikwe Jijini Dar Es Salaam alikofanyia kazi za kiuchungaji kwa miaka mingi ingetekelezwa, lakini kwa hiari na utashi wake alitaka azikwe Bukoba hivyo ni haki yake.
"Kila Askofu anawajibu wa kuchagua azikwe wapi, naye Kardinali Rugambwa alitaka azikwe Katika Kanisa Kuu la Bukoba, ni haki yake na hatimaye leo tunahamisha masalia yake na kwenda kuzika rasmi"alisema Askofu Ruwa'ichi.
Alisema kuhifadhiwa rasmi masalia yake katika kanisa hilo yatakuwa yakiombewa na waumini kutoka katika maeneo mbali mbali kutokana na jinsi alivyokuwa akithamini dini na kumtumikia Mungu.Alisema kupumzishwa si kwamba ni mahali pake bali ni sehemu alikoandaliwa na Mungu.
Alisema kazi kubwa ya Kardinali Rugambwa ilikuwa ni kuwaelekeza watu njia ya kwenda kwa Yesu.
Alisema katika mafundisho hayakuwa porojo bali alieneza habari njema za kumpenda, kumtumikia Mungu.
Hata hivyo baada ya misa hiyo yalianza maandamano ya magari na pikipiki ambayo yaliongozwa na Jeshi la polisi Mkoani Kagera ambapo maandamano hayo yalifika Bukoba mjini saa 9.00 alasiri huku jeneza lililobeba la Masalia yake likiwa la kifahari lenye namba ya usajili,T 607 BYX
Masalia ya Kardinali Rugambwa yaliwekwa karibuni saa 4.20 jioni na watu maalum waliokuwa wameandaliwa.
Aidha katika maziko hayo rasmi katika eneo la kaburi walioenda ni waandishi wa habari, maaskofu na baadhi ya mapadri waliokuwa na shughuli maalum pekee.
Askofu Ruwa’ichi aliwaongoza baadhi ya maaskaofu kuweka mashada ya maua katika kaburi la Kadinali Rugambwa, ambapo katika eneo alikozikwa jumla  kuna makaburi matatu.
Hata hivyo katika mazishi hayo hayakuweza kuwahiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambapo yeye alitua mjini hapa saa 4.30 jioni wakati maziko hayo yalianza saa 9.30 alasiri na saa 4.20 akapumzishwa katika nyumba yake ya milele.
Kutokana na uwingi wa watu waliofurika katika maziko hayo mjini hapa, magari yote yalioamuriwa kwenda kuegeshwa katika uwanja wa Kaitaba kulingana na maelezo yaliotolewa na Jeshi la polisi, ambapo hata watu waliokuwa wakiuza bidhaa mbali mbali walialimika kuuza zaidi ya mita 500 kutoka katika eneo la sherehe hizo.
Katika sherehe za maziko hayo wanaumini waliweza kushudia moja kwa moja kupitia screen za lungina zilizokuwa zimewekwa kila sehemu katika viwanja vya makanisa hayo, Kashozi na Bukoba mjini.
Hata hivyo idadi ya watu waliokuwa nje ya uwanja wa kanisa hilo  waliokosa nafasi ya kukaa ilikuwa sawa na watu waliokuwa ndani ya viwanja vya kanisa hilo.
Kardinali Rugambwa alizaliwa  Julai 12, 1912 katika kijiji cha Bukongo Rutabo Kamachumu wilayani Muleba katika familia ya kifalme na kufariki dunia mwaka 1997 akiwa na miaka 85.