Thursday, September 13, 2012

Kero na ghadhabu katika nchi za Kiarabu



Kero na ghadhabu katika nchi za Kiarabu

Kumezuka ghasia zaidi nje ya ubalozi wa Marekani mjini Cairo kati ya polisi na waandamanaji wanaokashifu filamu ambayo wanasema kuwa inakejeli imani ya Kiislamu.
Runinga ya Misri ilionyesha gari likiteketezwa moto na watu wengine wakikimbia vitoza machozi.

Taarifa zinazohusiana

Wakati huohuo maafisa wa Marekani wanasema serikali ya nchi hiyo inachunguza ikiwa mashambulio ya jumanne kwenye ubalozi wa Marekani katika mji wa Libya wa Benghazi yalikuwa ni ya kupangwa au la .
Balozi wa Marekani nchini Libya , Christopher Stevens, aliuawa .
Maafisa wa Marekani wameelezea mashambulio hayo kama yenye utata na yenye kupangwa kitaalamu na kuna tetesi kwamba makundi ya jihad huenda yalihusika .
Awali ilifikiriwa kuwa mashambulio hayo yalikuwa na uhusiano na maandamano ya kupinga filamu iliyokuwa inamkejeli Mtume Mohammed.
Takriban waandamanaji mia mbili wamekusanyika karibu na ubalozi wa Marekani mjini Cairo Misri kwa usiku wa pili kuelezea hasira yao juu ya filamu hiyo .

Aliyekuwa balozi wa Marekani nchini Libya Christopher Stevens
Awali waandamanaji walirusha mawe kwenye ubalozi huo na vikosi vya usalama vikafyatua mabomu ya kutoa machozi kuwa tawanya.
Watu wenye silaha waliokuwa na maguruneti walichomo moto jengo la ubalozi na walioshuhudia wanasema watu hao walizingira eneo hilo.
Rais Obama amelaani vikali shambulio hilo na ameahidi kushirikiana na serikali ya Libya kuwafikisha mbele ya sheria wahusika
SOURCE: http://www.bbc.co.uk/swahili/habar

'Innocence of Muslims' Trailer Part 7 [HD] - Egypt Protest Film

'Innocence of Muslims' Trailer Part 6 [HD] - Egypt Protest Film

'Innocence of Muslims' Trailer Part 6 [HD] - Egypt Protest Film

Kilichopelekea Balozi wa marekani Libya kuuwawa ni hiki ('Innocence of Muslims' Trailer Part 2 [HD] - Egypt Protest Film)

Wednesday, September 12, 2012

ONLY IN TANZANIA!


"ONLY IN TANZANIA!

   Yapo Maajabu mengi sana...Ila Maajabu Makuu Yaliyopo Tanzania ni Haya hapa;
     

 1. Mmoja wa Majaji Walioteuliwa kwa Mujibu wa Tundu Lissu Kumbe ndo
    kwanza anasoma shahada so darasani nae anasoma"What is Law of      Torts" then anapata SUP...U can Only find in TZ....afu mwalimu wake ni advocate inakuwaje akimpelekea kesi Jaji wa aina hiyo??

 2. Serikali Makini ambayo sio dhaifu ina Watumishi Hewa 9,949
    wanaopata Mshahara ambao Jumla ya hela inayopotea ni kama Bil 70
    ambazo zingetumika kulipa Madaktari na walimu, lakini Serikali
    inasema haina hela, hawana hela ya kulipa walimu na Madaktari ila
    wanazo za Watumishi hewa...Only u can find in TZ.

 3. Serikali Ya Uingereza Ilirudisha Chenji ya RADA, Serikali ikasema
    hela inapeleka Kununulia Vitabu kwa Ajili ya Shule Nchi nzima, Kumbe Kampuni iliyopewa tenda ya Kusambaza Vitabu nchi nzima ilitoa rushwa ya US$ 500,000 kupata tender Serikali ya Uingereza imeifungia miaka 7, You Can Only find in TZ.

4. Wanafunzi Waliofaulu Darasa la Saba get me well waliofaulu darasa
   la 7 kwenda Sekondary Hawajui Kusoma wala Kuandika, Je waliofeli
   Watakuwa hawajui kufanya nini??...You Can Only Find In Tanzania
  
  5. Washiriki wa Michezo ya Kimataifa (sijataja Mchezo wala
     mashindano) wako watano (5) lakini wanaowasindikiza Washiriki wako 12 You can Only find in Tanzania......

 6. Sehemu Pekee ambaye Mtu uliyetaka Kumdhuru kwa Kukusumbua then
    unaomba Umlinde (refer to Dr. Ulimboka's Case)..Yaani Mbwa Mwitu
    anaomba kazi ya Kulinda Mbuzi......You Can Only find in Tanzania..

  7.Only in Tanzania serekali inaweza kabisa kulipisha watu ushuru wa sticker ya fire Bila kuuliza kama una huo mtungi wa kuzimia moto wala kukagua gari wala kukupa hiyo sticker Na wananchi wake wakakubali na kunyamaza tu.

  8. Only in Tanzania hata rais hajui ni kwanini raia wake ni masikini?

       
Yapo Maajabu Mengi sana Lipi nimesahau???" Ongezea Moyoni
Source: http://just90.justhost.com/mailman/listinfo/members_nwb.or.tz

Rais mpya wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud , amenusurika jaribio la kumuua mjini Mogadishu.Milipuko miwili imetokea nje la lango la makao ya rais huyo katika hoteli ya Al-Jazeera wakati rais huyo alipokuwa anajiandaa kufanya mkutano na waandishi wa habari.Taarifa zinasema kuwa waziri wa mambo ya nje wa Kenya Sam Ongeri pia alikuwa katika hoteli hiyo wakati wa shambulizi. Hata hivyo wawili hao wamenusurika. Inaarifiwa watu wanne wameuawa na wengine watatu kujeruhiwa.

Chanzo:http://www.bbc.co.uk/swahili/habari

Thanks Nick Jerry for the Video about "Innocence of Muslims Trailer 2..."

Balozi wa Marekani Nchini Libya Bw Christopher Steven Auawa

Balozi wa Marekani Nchini Libya Auawa leo Kwa sababu ya kumkashifu Mtume Muhamad

BENGHAZI, Libya (Reuters) - The U.S. ambassador to Libya and three other embassy staff were killed in a rocket attack on their car, a Libyan official said, as they were rushed from a consular building stormed by militants denouncing a U.S.-made film insulting the Prophet Mohammad. Gunmen had attacked and burned the U.S. consulate in the eastern city of Benghazi, a center of last year's uprising against Muammar Gaddafi, late on Tuesday evening, killing one U.S. consular official. The building was evacuated. The Libyan official said the ambassador, Christopher Stevens, was being driven from the consulate building to a safer location when gunmen opened fire. "The American ambassador and three staff members were killed when gunmen fired rockets at them," the official in Benghazi told Reuters. There was no immediate comment from the State Department in Washington. U.S. ambassadors in such volatile countries are accompanied by tight security, usually travelling in well-protected convoys. Security officials will be considering whether the two attacks were coordinated. Libyan deputy prime minister Mustafa Abu Shagour condemned the killing of the U.S. diplomats as a cowardly act. The consular official had died after clashes between Libyan security forces and Islamist militants around the consulate building. Looters raided the empty compound and some onlookers took pictures after calm returned. In neighboring Egypt, demonstrators had torn down an American flag and burned it during the protest. Some tried to raise a black flag with the words "There is no God but God, and Mohammad is his messenger", a Reuters witness said. PORTRAYAL OF PROPHET U.S. pastor Terry Jones, who had inflamed anger in the Muslim world in 2010 with plans to burn the Koran, said he had promoted "Innocence of Muslims", which U.S. media said was produced by an Israeli-American property developer; but clips of another film called "Mohammad, Prophet of Muslims", had been circulating for weeks before the protest. That film portrayed Mohammad as a fool, a philanderer and a religious fake. In one clip posted on YouTube Mohammad was shown in a sexual act with a woman. Jones, a pastor in Florida whose latest stunt fell on the anniversary of the September 11, 2001, attacks on the World Trade Center and the Pentagon, triggered riots in Afghanistan in 2010 with his threat to burn the Koran. Many Muslims consider any depiction of the Prophet offensive and any depiction of him can cause outbursts of anger in the Islamic world and among Muslims in Europe. Libya's interim government has struggled to impose its authority on a myriad of armed groups that have refused to lay down their weapons and often take the law into their own hands. It was clearly overwhelmed by Tuesday night's attack on the consulate that preceded the assault on the ambassador. "The Libyan security forces came under heavy fire and we were not prepared for the intensity of the attack," said Abdel-Monem Al-Hurr, spokesman for Libya's Supreme Security Committee. In Benghazi, unidentified men had shot at the consulate buildings, while others threw handmade bombs into the compound, setting off small explosions. LOOTED On Wednesday morning, the compound stood empty, with passers-by freely walking in to take a look at the damage. Walls were charred and a small fire burned inside one of the buildings. A small group of men was trying to extinguish the flames and three security men briefly surveyed the scene. A Reuters reporter saw chairs, table and food lying alongside empty shells. Some blood stains could also be seen in front of one of the buildings. Three cars were torched. The crowd of around 2,000 protesters in Cairo was a mixture of Islamists and teenage soccer fans known for fighting police and who played a part in the revolt that toppled Egypt's leader Hosni Mubarak last year. The fortress-like U.S. mission is near Tahrir Square, where Egypt's uprising began and the scene of many protests since. Youths danced and chanted football songs. A Reuters reporter said they appeared to climb into the embassy compound almost as an afterthought. "We sacrificed dozens and hundreds during the uprising for our dignity. The Prophet's dignity is more important to us and we are ready to sacrifice millions," said mosque preacher Mohamed Abu Gabal who joined the protest. U.S. Secretary of State Hillary Clinton, in a statement late on Tuesday, confirmed the death of the U.S. consular diplomat in Libya, who was not identified, and condemned the attack there; but she made no mention of an attack on the Ambassador's car. (Additional reporting by Hadeel Al Shalchi in Tripoli, Sarah N. Lynch and Arshad Mohammed in Washington, and Reuters reporters in Cairo and Benghazi; Writing by Edmund Blair and Tom Pfeiffer; editing by Ralph Boulton and Janet McBride)

Obama ana bahati kuwa na mke kama Michele

Rais Obama akitoa hotuba ya kukubali kugombea tena Urais 2012

Tuesday, September 11, 2012

Barrel Bombs could be used as WMD!

Mwangosi aliuliwa hivi

Mwangosi aliuawa hivi
• SIMULIZI YA SHAHIDI

na Mwandishi wetu
SEPTEMBA 2, 2012, polisi waliua kikatili mwandishi wa habari wa kituo cha Channel Ten, Daudi Mwangosi, katika Kijiji cha Nyololo, mkoani Iringa. Alikufa mbele ya Kamanda wa Polisi mkoani humo, Michael Kamuhanda, wakati polisi hao walipovamia ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ili kuwatawanya wasifungue tawi la chama chao katika kijiji hicho.
Mmoja wa watu walioshuhudia tukio zima, ni mwandishi wa Tanzania Daima, Abdallah Khamis. Ifuatayo ni simulizi ya kile alichokiona wakati polisi wanaondoa uhai wa Mwangosi.
SIKU hiyo asubuhi tulipata taarifa kuwa Kamanda wa Polisi mkoani humo (RPC), Michael Kamuhanda, alipanga kukutana na waandishi wa habari majira ya saa 2.30 ambapo waandishi walifika akiwemo Daudi Mwangosi.
Tukiwa katika chumba cha mikutano katika jengo la polisi Mkoa wa Iringa, Kamanda wa mkoa huo, alifika akiongozana na maafisa wake wawili na kuanza kutusomea taarifa ya zuio la mikutano ya CHADEMA iliyokuwa iendelee siku hiyo baada ya kupisha zoezi la awali la sensa.
Alitusomea zuio hilo na kutuambia hata viongozi wa CHADEMA wameshataarifiwa usiku wa Septemba Mosi. Tukamuuliza mbona taarifa za sensa zinaeleza kuwa kuna mafanikio kwa asilimia 95 na waliobaki wanatakiwa waende kwa viongozi wao? Akatujibu kuwa hilo ni agizo na linapaswa litekelezwe na CHADEMA.
Waandishi hawakuchoka kumuuliza maswali RPC na moja ya maswali yaliyoonekana kumkera kamanda huyo ni lile lililotoka kwa Daudi Mwangosi kuwa mbona wakati wa mwanzo walipozuia mikutano ya CHADEMA mkoani humo mikutano mingine ya CCM ndani ya mkoa huo na sehemu nyingine nchini ilikuwa inaendelea.
Swali lingine la Mwangosi lilimtaka kamanda huyo kutumia busara katika hali iliyopo kwa lengo la kuepusha maafa yanayoweza kutokea endapo angeendelea kushikilia msimamo wake kuwa hakuna mkutano wa aina yoyote utakaofanyika.
Baada ya maswali hayo, tulimuona Kamanda Kamhanda akiwa amekunja sura kama ishara ya kuchukizwa na maswali ya Mwangosi ambaye aliongeza swali lingine kwamba, “inaonekana Kamanda umechukia kutoka ndani ya moyo wako” na kamanda akajibu “ni lazima nichukie na nawachukia hawa CHADEMA kwa kuwa ninaipenda kazi yangu na pia ninakaribia kustaafu na sitaki kustaafu vibaya.”
Baada ya hapo maafisa waliokuwa na RPC waliandika ujumbe kwenye karatasi na wakamfikishia mkuu wao, na baada ya muda mkutano huo ulimalizika huku kukiwa na kauli za utani wa hapa na pale kati ya waandishi wa habari na baadhi ya askari juu ya kwenda kuripoti matukio ya siku hiyo.
Tulipokuwa nje ya jengo, Mwangosi, kwa kuwa ni mwenyeji wa mkoa huo, alikuwa akitaniana na mmoja wa askari aliyevaa kiraia, ambaye alimwambia kuwa, “huko hakutakuwa na kujuana na kuna uwezekano wa watu kufa.”
Mwangosi alijibu papo hapo kuwa hilo haliogopi kwa kuwa kifo ni ada ya mja yeyote na kwamba ataogopa kama mtu atamuahidi kuishi milele.
Baada ya hapo, kila mmoja alitawanyika katika eneo lake, na majira ya saa saba mchana baadhi ya waandishi walikutana ili kuanza safari katika Wilaya ya Mufindi kwa ajili ya kuripoti mkutano wa ndani wa CHADEMA na ufunguzi wa matawi.
Waandishi wa habari hao pamoja na mimi ni Godfrey Mushi (Nipashe), Olver Motto (Star Tv), Renatus Mutabuzi (ITV), Clement Sanga (Mwananchi), Joseph Senga (Tanzania Daima) na Tumaini Makene (Ofisa Habari wa CHADEMA).
Tulipofika katika mji wa Mafinga, tulipata chakula cha mchana kabla ya kwenda katika Kijiji cha Nyololo, na muda wote huo Mwangosi alikuwa hajaungana nasi.
Tuliondoka Mafinga kuelekea Nyololo huku mwenzetu Clement Sanga akiwasiliana na Mwangosi aliyesema yuko katika basi na angeungana nasi tukiwa Nyololo. Tulipofika pale tuliona askari wachache wakiwa wamesimama barabarani huku gari lao moja likiwa linajaza mafuta katika kituo cha mafuta kilichopo eneo hilo.
Tukiwa njia ya kwenda Mbeya, mita kama 100 kutoka katika mji wa Nyololo, kushoto kwetu tuliziona ofisi za CHADEMA zikiwa zimepambwa kwa bendera nyingi, na kulia kwake tuliona magari manne ya askari waliokuwa na silaha.
Baada ya kupita eneo hilo, gari moja la polisi lilikuwa likitufuata, na hapo tulishauriana kugeuza gari kurudi katika eneo la mji. Tulipofanya hivyo, na gari la polisi lilisimama.
Wakati tunarudi katika eneo la mji, tuliegesha gari pembeni. Baadhi ya waandishi wa habari waliingia mitaani kwa makubaliano kuwa baada ya dakika 10 tuwe tumerejea kwa ajili shughuli iliyotuleta - kushuhudia ufunguzi wa tawi hilo jipya la CHADEMA.
Muda huo ulipofika, tulirejea, lakini Mwangosi alikuwa hajaungana nasi. Baadaye tulianza kuona baadhi ya magari yakiwa na bendera ya CHADEMA yakipita moja baada ya jingine.
Kuwasili kwa Mwangosi eneo la Nyololo
Saa 10.22 Mwangosi aliwasili kwa basi ambalo sikumbuki kama ni Hood au Abood; na muda huo huo tukawaona askari wakiyatoa magari yao kutoka mafichoni na kuingia upande wa kulia wa mji wa Nyololo kwenye ofisi za kata za CHADEMA.
Wakati askari wakiwa wanapita walikuwa wakisema Dk. Slaa anatokea eneo la Wami. Waandishi wa habari wakawa wamejiandaa kwenda kwa kufuata njia hiyo.
Tuliegesha gari letu mbali. Mwangosi ambaye hakuwepo awali, akataka kuchukua pikipiki ili awahi. Kwa kuwa muda huo nilikuwa naye, nikamsihi kuwa hana haja ya kuingia gharama kwa kuwa gari la waandishi wa habari lipo. Akanielewa, na tukaingia katika gari hilo, huku akiwa amempakata Oliver Motto wa Star Tv.
Tulipoenda kama mita 50 hivi, tulikutana na msafara wa CHADEMA ukiwa unaelekea tunakotoka. Gari la waandishi wa habari na magari ya polisi yakalazimika kukaa pembeni kuyapisha, kisha wakaungana nao kuelekea katika ofisi za tawi za chama hicho.
Ofisi za tawi za CHADEMA katika mji huo wa Nyololo zipo mita zaidi ya 100 upande wa kushoto wa bararara ya kuelekea Mbeya. Awali polisi walikuwa wameegesha magari yao barabarani wakati CHADEMA wakielekea katika ofisi zao.
Hakukuwa na vurugu yoyote. Ghafla kiongozi wa polisi ambaye alikuwepo pale - tulimtambua kwa jina la Mnunka - aliwaamuru askari wake watoe ilani kwa kunyoosha bendera kubwa nyekundu juu na kuwataka CHADEMA waondoke katika ofisi zao. Tukapiga picha tukio hilo.
Wakati askari wakijiandaa kuwafuata wana CHADEMA katika ofisi zao, alitokea mtu aliyevaa shuka na kujifunga kitambaa kichwani ambaye baadaye alijitambulisha kama mkuu wa upelezi mkoa (RCO), akawaamuru wenzake waende katika ‘target’ lakini wasithubutu kutumia nguvu bila amri.
Hapa ndipo tulipoanza kupata wasiwasi ni nani anatoa amri kwa kuwa yule wa mwanzo, Mnunka alijiapiza kuwa wamechoka kuvumilia, na kwamba siku hiyo CHADEMA watawatambua. Hata tulipomuuliza maana ya kauli ile, hakutupa jibu la kueleweka.
Katika hali hiyo, mtu aliyejitambulisha kama ndie RCO alizungumza na viongozi wa CHADEMA, wao wakamwambia wako katika kikao cha ndani. Yeye akasema jukumu lake ni kuhakikisha usalama unakuwepo, na kwamba kama ni suala la kikao cha ndani hawawezi kuzuia.
Tulitaka kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali kutoka kwa RCO ambaye alikuwa akizungumza kwa simu na mtu ambaye baadaye ilikuja kubainika kuwa ni Kamanda wa Polisi wa Mkoa (RPC), akawa anamueleza kuwa hali ni salama. Alituahidi waandishi wa habari tuvute subira “kwa kuwa mwenye mkoa amewasili.”
Baada ya kuwasili kwa RPC Kamuhanda, Kamanda wa FFU, Mnunka alienda akamnong’oneza jambo. Pale pale, Kamuhanda akaonekana kukasirika. Akaagiza CHADEMA wasimamishe shughuli yao mara moja.
Tulitaka kujua tafsiri ya mkutano wa ndani kwa Jeshi la Polisi ni ipi, ni kwa wahusika kukaa ndani au ni ule mkutano utakaowahusisha wanachama peke yao kama ambavyo CHADEMA walikuwa wanasema pale. RPC akatujibu kuwa hilo halielewi na yeye si mwanasiasa.
Baada ya maelezo hayo, waandishi wa habari tulimbana RPC kwa maswali hata ikafikia hatua ya kamanda huyo kuanza kuwanyooshea vidole baadhi yetu, huku alimlalamikia Mwangosi kwamba kwanini hakushiba na majibu aliyopewa tangu asubuhi.
RPC akaniambia mimi kwamba nauliza maswali yanayopingana na mtazamo wa jeshi hilo; akamwambia Mutabuzi kuwa anamfahamu.
Baada ya hali hiyo, CHADEMA walimaliza mkutano wao katika ofisi za tawi na wakawa wanaelekea katika ofisi za kata. Gari lililotubeba lilikuwa nyuma ya gari la RPC ambaye baadaye dereva wake aliendesha kwa kasi kwenda mbele kutaka kuzuia msafara wa CHADEMA.
Lakini viongozi wa CHADEMA walikuwa wameshafika katika ofisi yao ya kata na tukashuka kwenda kushuhudia kinachoendelea. Hapo ndipo tulimkuta Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zanzibar, Hamad Yusuph na viongozi wengine wakisaini katika kitabu cha wageni.
Ghafla, RPC akatoa amri ya kuwakamata viongozi wa CHADEMA waliokuwa katika ofisi yao. Baada ya amri hiyo, wanachama wa CHADEMA waliokuwa pale wote walikaa chini wakinyoosha mikono juu.
Balaa linaanza kwa amri ya RPC Kamuhanda
Baada ya RPC kutoa amri hiyo, polisi walioipokea walianza kurusha mabomu ya machozi kuelekea sehemu waliyokaa wanachama wa CHADEMA. Mabomu hayo yalirushwa na kuumiza wengi, wakiwamo waandishi wa habari. Mimi nilipigwa na kitu chenye kishindo, nikajeruhiwa mkono wa kushoto na sehemu ya paja la mguu wa kulia.
Jitihada za polisi kuwatawanya wafuasi wa CHADEMA zilifanikiwa. Baadhi ya watu na viongozi waliwekwa chini ya ulinzi, sisi tukiwa tunaendelea kufanya kazi yetu ya kukusanya taarifa ili kuhabarisha umma juu ya kile kinachoendelea katika eneo hilo.
Wakati hali hiyo ikiendelea, ofisi za kata za CHADEMA hazikuwa na mtu. Askari wakawa wanapiga mabomu kuelekea ndani ya ofisi hiyo tupu.
Tuliendelea kupiga picha tukio hilo. Ghafla askari mmoja akamgeukia mwandishi wa gazeti la Nipashe, Godfrey Mushi, akaanza kumpiga.
Baada ya kuona mwandishi huyo anapigwa, Mwangosi aliwasogelea askari akitaka kujua sababu za kumshambulia mwandishi wakati yupo kazini kama ambavyo askari hao walivyokuwa wakiwajibika.
Swali la Mwangosi likavuta askari wengine. Wakamzunguka na kuanza kumpiga kwa marungu, mateke na ngumi. Wakati hayo yakifanyika, RPC alikuwa pale anashuhudia.
Baada ya kuona kipigo kimekuwa kikali, Mkuu wa Kituo cha Polisi (OCS) cha Mafinga aliingilia kati kutaka kumnusuru Mwangosi.
Wakati Mwangosi akiwa anashambuliwa, mpiga picha wa gazeti la Tanzania Daima, Joseph Senga, naye alikuwa katika wakati mgumu baada ya askari kumdhibiti na kuanza kumpekua mifukoni, huku mwenyewe akijitahidi kujinasua mikononi mwao.
Mbali na mimi na Senga, muda huo hakukuwa na raia yeyote katika eneo lile, isipokuwa Godfrey Mushi wa Nipashe ambaye sina hakika kama alikuwa anafahamu kinachoendelea maana alikuwa amepigwa sana, yuko hoi.
Baada ya kuona kipigo kinazidi kwa Mwangosi huku Senga akiendelea kupiga picha, uzalendo ulinishinda, nikaamua kumfuata Kamanda wa Polisi mkoani humo aliyekuwa mita zisizozidi kumi ndani ya gari lake, akishuhudia tukio lile. Nikamuomba asaidie kumnusuru Mwangosi na kipigo kile.
RPC alishusha kioo cha gari lake, akaniangalia, kisha akafunga kioo, huku dereva wake akawa anapiga honi. Sikujua maana ya honi hiyo.
Baada ya kuona hakuna msaada wowote kutoka kwa RPC, nilisogea karibu kwa ajili ya kuendelea kupata picha ya tukio, ili umma ujue juu ya madhila yanayowapata waandishi wa habari mikononi mwa polisi.
Wakati nikiwa naendelea kuchukua picha, nilimwona askari mmoja akinyoosha mkono juu na mwingine aliyevaa kiraia akiwa ameshika bastola yake kuelekeza juu, huku wengine wakiwa wanaendelea kumpiga Mwangosi aliyekuwa anajitahidi kuinuka kwa kumshika mmoja wa askari wale.
Katika harakati za Mwangosi kujinasua, nilimshuhudia mmoja wa wale askari akiwa kama anainama akaelekeza mtutu wa bunduki usawa wa tumbo la Mwangosi aliyekuwa katika hali ya kutaka kusimama huku akipiga kelele “msiniuee, msiniuee…”
Mara nikasikia mlipuko mkubwa pale pale walipo; baadhi ya nyama zikarushwa na kutapakaa, nyingine zikanirukia mimi na kuchafua fulana yangu.
Kumbe walikuwa wamemlipua Mwangosi! Nikapiga picha ya mwili uliosambaratika na kukatika vipande vipande. Nikaona askari wale wanambeba askari ambaye naye alijeruhiwa na mlipuko uliomuua Mwangosi. Nikakimbia kujinusuru na askari wale.
Sikuona tena usalama wangu mbele ya polisi wake. Sikumwamini tena RPC kama angeweza kulinda maisha yangu. Nikatimua mbio kuelekea nisipopajua.
Nikiwa nakimbia nilichomoa kadi ya kamera kutoka katika kamera yangu ili nisipokonywe. Hapo ndipo nilipokutana na mwandishi mwingine, Francis Godwin, nikamwambia asielekee nilikokuwa natoka mimi – ambako ndiko alikuwa anataka kwenda - kwa kuwa Mwangosi ameshauawa na polisi!
Wakati naachana na Godwin, nilichukua simu yangu na kumpigia Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda, ambaye ndiye Mhariri Mtendaji wa gazeti hili kwa ajili ya kumpa taarifa. Bahati mbaya simu yake haikupokelewa.
Nikamfuata Makene (Tumaini, afisa habari wa CHADEMA) aliyekuwa amejikinga katika gogo, alikokuwa pamoja na Oliver Motto, nikawaambia eneo hili halitufai watatuua. Ndipo nikampigia simu Bakari Kimwanga, mwandishi wa gazeti la Mtanzania, nikamfahamisha kuwa Mwangosi ameuawa na polisi. Tukakimbilia porini kujificha, kila mtu akiwa analia kivyake.
Baada ya kukaa porini kwa muda, tuliamua kubadilisha nguo zetu ili tusitambulike kirahisi. Tukatoka mafichoni kuangalia hali ya usalama. Tukaanza kuwatafuta wenzetu ambao tulipoteana nao. Baadaye tulikodi teksi kuwafuata wenzetu ambao wakati huo walishakimbia kutoka eneo hilo la hatari.
Tukiwa katika hoteli ya MR mkoani Iringa, mwananchi mmoja alikuja kutueleza kuwa alifanikiwa kukusanya sehemu ya mwili wa marehemu Mwangosi pamoja na mabomu yaliyoachwa katika eneo la tukio na walipoangalia wakaona ni sehemu ya nyama ya utumbo iliyowekwa katika mfuko pamoja na mabomu ya machozi na kuyapanga yale mabomu juu ya meza ya hoteli hiyo na kuyapiga picha huku utumbo wa Mwangosi ukiendelea kuwa katika mfuko uliowekwa.
Hadi sasa sijajua endapo sehemu hiyo ya utumbo ilizikwa usiku ule mkoani Iringa au uliunganishwa na sehemu nyingine ya mwili wake uliotawanywa na bomu hilo kiasi cha kushindwa kujua kama ni mwili wa binadamu au ni ng’ombe aliyechinjwa tayari kwa mauzo.
Hivi ndivyo tulivyompoteza mwandishi mwenzetu, Daudi Mwangosi, akiwa mikononi mwa polisi

Source: www.wanabidii.net

Maazimio Ya Kikao Cha Kamati Kuu ya CHADEMA

1.Uwajibikaji wa kisiasa wa viongozi wa serikali na idara zake.,Waziri
Emmanuel Nchimbi,IGP Mwema,Paul Chagonja,RPC Morogoro na Kamanda wa
FFU,na RPC IRINGA na Kamanda wa FFU wajiuzulu na au wafukuzwe kazi

2.RPC Morogoro na Iringa,makamanda wa FFU Morogoro na Iringa,na
maaskari waliouwa wakamatwe mara moja na kufunguliwa mashitaka

3.Rais aunde tume huru ya uchunguzi wa vifo tata katika matukio ya
kisiasa.1.ARUSHA vifo 3.IGUNGA,vifo vingi havijulikani bado,3.ARUMERU
MASHARIKI,vifo 5, 4.SINGIDA kifo 1, MOROGORO na IRINGA
chadema haitatambua wala kushirikiana na kamati batili ya NCHIMBI.

4.Msajili wa vyama vya siasa John Tendwa ni mtu hatari kwa taifa kwa
kauli tata anazozitoa.anashirikiana na au anajipendekeza kwa CCM na
Serikali yake.CHADEMA tangu sasa haitafanya kazi na Tendwa wala
kufanya mawasiliano naye ya kiofisi.Labda kama atagundua makosa yake
na kuomba msamaha,chadema itatafakari namna ya kufanya naye kazi tena.

5.TBC TAIFA Television na Redio ni hatari kwa taifa,kwa kubobea
kupotosha umma juu ya matukio mengi.Hivyo CHADEMA Inatangaza mgogoro
na TBC na inaelekeza na kuomba wanachama ,wapenzi,na wananchi wote
wapendao ukweli na haki,kuisusia TBC

6.Jeshi la Polisi lijue kuwa Maandamano ndiyo siasa yenyewe na
mikutano ya hadhara ni lazima kwa mawasiliano ya umma na siasa.kuzuia
vitu hivyo ni kunyima wananchi haki yao ya kikatiba ya uhuru wa
kukusanyika na kutoa maoni,pia kupata habari na taarifa

7.Operesheni MOVEMENT FOR CHANGE M4C,Inaendelea kadiri ya ratiba
ilivyopangwa katika utaratibu uleule uliokuwepo awali.Inarejea Iringa
Siku si nyingi.Na kamati kuu Imetoa msisitizo MAALUM kwa jimbo
mojawapo singida,ambapo wamesema watatumia helcopita,magari,pikipiki
na baiskeli na miguu,na badala ya kupita vijijini kama majimbo
mengine,Chadema wanasema kwa sababu maalum katika jimbo hilo watapita
kitongojikwa kitongoji,ili kufunza adabu baadhi ya viongozi (msisitizo
ni wa msoma MAAZIMIO.jimbo hili laweza kuwa la Mwigullu Mchemba,kadiri
ya wanahabari waliokuwepo)

8.Kutokana na mgogoro wa muda mrefu mkoani mwanza uliosababisha meye
wa chadema kuvuliwa umeya kinyume na utaratibu na kwa njama za CCM na
Serikali,na bahati mbaya sana kwa kushirikisha madiwani wa
CHADEMA,KAMATI KUU imewavua UANACHAMA madiwani wake wawli 1 ADAMU
CHAGULANI wa kata ya IGOMA na HENRY MATATA wa KITANGIRI, PIA uongozi
wote wa CHADEMA mkoa wa mwanza Umevunjwa.

Imesomwa na
Mwenyekiti CHADEMA Taifa
Source: www.wanabidii.net

Importance of Making Love in a Relationship

Malawi’s popural evangelist Linly Mbeta captivated her audience as she explained to them about the importance of making love in a relationship and satisfying one another.
Mbeta, head of Chingonjetso Women’s Ministry based in Mbayani, one of the squatter townships in commercial city of Blantyre, said making love was beautiful and holy and therefore couples should not be afraid of satisfying one another.
She said couples or families should enjoy making love, saying sex is an act that must be learnt and developed.
“Satisfy each other in bed and avoid having sex outside marriage,” Mbeta said as quoted by the Weekend Times.
The preacher said sex enhanced love between husband and wife and therefore it should be done with a meaning.
“What is the problem? Wives, let us enjoy sex with our husbands, let us enjoy sex with our wives,” she said.
More rounds
Mbeta said couples should not sanction each other when it came to making love as this would cause a conflict in a family.
“Agree, if one wants more rounds, then go for it and in that way we won’t see husbands or wives enjoying sex outside,” she said.
The preacher pointed out that it important that as a couple they should communicate in order to satisfy each other and also meet one another’s needs especially when it comes to sex.
She emphasised that married couples should try and understand each other and address their differences at all times in order for their families to be fruitful.

Source from WWW.WANABIDII.NET

http://www.nyasatimes.com/malawi/2012/09/08/malawi-preacher-gives-couples-sex-tips-do-more-rounds/

Friday, September 7, 2012

SIKILIZA Dayna - Nivute Kwako

ASKARI watano wamekamatwa


ASKARI watano wa Jeshi la Polisi akiwamo anayetuhumiwa kumlipua kwa bomu Mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, marehemu Daud Mwangosi wamekamatwa na wanaendelea kuhojiwa na jeshi hilo mkoani Iringa.

Taarifa ya kukamatwa kwa askari hao imekuja siku moja baada ya kubainika kwamba, askari kadhaa walioendesha operesheni dhidi ya wafuasi wa Chadema mkoani Iringa na kusababisha kifo cha Mwangosi walitoka mikoa ya Dodoma, Mbeya na Morogoro.

Taarifa za uhakika zilizolifikia gazeti hili jana na kuthibitishwa na baadhi ya askari polisi mkoani Iringa na Makao makuu jijini Dares Salaam, zilisema kuwa polisi hao, akiwamo yule aliyeonekana kwenye picha za video na za mnato akimlipua kwa mtarimbo wa bomu la machozi (jina tunalo) wamekamatwa na kushikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Iringa.